Header Ads

WALEMAVU WAPEWA ELIMU YA MAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI


Mbeya. Katika harakati za kupunguza mambukizi ya virusi vya Ukimwi nchini,Hosptari ya Rufaa Kanda ya Mbeya  imendesha elimu ya tohara na mambukizi ya virusi vya Ukimwi kwa walemavu wa kusikia wanaoishi mkoani hapa.

Akizungumza kwenye  mafunzo hayo juzi, mratibu wa tohara kwa wanaume hosptali ya Rufaa Majuni Mtagwaba alisema wamefikia hatua  ya kutoa elimu kwa walemavu hao baada ya viongozi wa Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) Mkoa wa Mbeya kupeleka maombi ya kupatiwa elimu hiyo.


Mtagwaba alisema baada ya hosptali kupata maombi hayo ,waliona kuna haja ya kutoa elimu hiyo kwani makundi ya walemavu yamekuwa hayapati elimu hiyo kutokana changamoto ya mawasiliano, hivyo kupelekea walemavu kukumbwa na mambukizi magonjwa   mara kwa mara kama kisonono,kaswende, gonolea pamoja na ukimwi.

“Makundi ya walemavu hasaViziwi wamekuwa kinara wa kufanya ngono zembe kutokana na kutokuwa na elimu ya  kujikinga na mambukizi ya ukimwi na mwitikio wa kufanyanyiwa tohara haupo kabisa,ndiyo maana wemekuwa wakiambukizwa mara kwa mara”,alisema.

Alisema,tohara kwa wanaume inapunguza mambukizi yanayotokana na ngono kwa asilimia 60,ndiyo maana tumekuwa tukihamasisha wananchi kujitokeza kufanyiwa tohara.s

Katibu wa chama cha viziwi Mkoa wa Mbeya Queen Majembe alisema mafunzo hayo ni mara ya kwanza kupata kwa walemavu hao na yamekuja muda mwafaka kutokana na kipindi hiki mambukizi ya virusi yameshika kasi katika maeneo mbalimbali nchini.

Queen alisema,Mkoa wa Mbeya una viziwi 7,000 na wengi hawana elimu ya tohara pamoja na mambukizi ya virusi vya ukimwi hivyo ni vema taasisi mbalimbali zijitokeze kuhamasisha elimu hiyo ili kunusuru jamii ya walemavu.

“Tunaishukuru Hosptali ya Rufaa kwa kutupatia elimu hii ambayo itatusaidia kwa kiasi kikubwa katika jamii tunazotoka lakini pia tutaisambaza kwa walemavu  ambao hawajafika hapa leo hasa waliopo wilayani”,alisema.

Naye mlemavu Epafula Isaya alisema,awali walikuwa wanashindwa kwenda vituo vya afya  kufanyiwa tohara kwani hawajahi kupewa elimu ya faida za kufanyiwa tohara na hasara zake.



No comments