Header Ads

BUSOKELO WAJENGA SOKO LA NDIZI LA KISASA


Mbeya. Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Busokelo mkoani hapa Eston Ngilangwa amewagiza watendaji wa kata na vijiji kusimamia na kuhakikisha wakulima wa zao la ndizi hawauzi kiholela na badala yake wapeleke kwenye soko lililo jengwa hivi karibuni.

Akizungumzia hatua jana jijini hapa Ngilangwa alisema halmashauri ifikia hatua kujenga soko la ndizi katika kata ya Lupata kutokana na hujuma za wafanyabiashara kwa wakulima wa zao hilo.

“Kutokana na ujenzi wa soko hili nimeagiza watenadaji wangu wawe ndiyo wasimamizi wa kuhakikisha mkulima anapeleka  ndizi zake soko la Lupata na hukuna mkulima atakaeruhusiwa kuuza ndizi mashambani kama ambavyo walizoea hapo awali hivyo wanatakiwa wapeleke sehemu ambapo serikali tumepanga”alisema.

Ngilangwa alisema kwanzishwa kwa soko hilo halmashauri itaweza kuwathibiti wafanyabiashara ambao walikuwa wanakwepa kulipa ushuru na kuwarubuni wankulima kwa bei za ajabu.

Makamu mwenyekiti wa Halmashauri hiyo ambaye pia ni Diwani wa kata ya Lupata Uswege Mbamba alisema ujenzi wa soko hilo utasaidia wakulima kunufaika kilimo chao kwani serikali itaweka bei elekezi ambapo mkungu mmoja utauzwa sh12,000 kutoka 6,000 ya awali.

“Lengo la halmashauri kujenga soko hili ni kutaka wakulima wanufaike na kilimo cha zao la ndizi kwani wakulima walikuwa wanauza bei ambazo zilikuwa hawazinufaishi”alisema.

Mbamba aliongeza kuwa licha ya kujenga soko hilo lakini wananchi watahamasishwa  kuongeza uzalishaji wa zao hilo ili wakati wote ziwe zinapatikana sokoni hapo,ikiwa ni sambamba na kuwaelimisha faida za uwepo wa soko hilo. 

Akiongea hivi karibuni mkulima wa zao hilo kutoka kijiji cha Lusungo Bernad Mwansepe alisema ujenzi wa soko hilo utaleta ukombozi kwa mkulima mmoja mmoja kutokana na madarali kuthibitiwa.

“Tunaipongeza halmashuri yetu kwa hatua waliyofikia ya kutaka wakilima kwanza kunufaika na zao tunalo lima,na sisi kama wakulima tutongeza juhudi ya uzalishaji wa ndizi kwa wingi kwani ukombozi umefika”alisema.

Mwansepe aliongeza kuwa Serikali waongeze maofisa organi katika vijiji kwa ajili ya kuwapa elimu ya kilimo cha kisasa wazalishaji,kwani ni kwa mda mrefu wamekuwa wakiendesha shughuli za kilimo bila kupata ushauri kutoka kwa watalamu. 

No comments