KABAKA AFANYA ZIARA MBEYA
KABAKA AFANYA ZIARA MBEYA
Mbeya. Chama Cha Mapinduzi kinatarajia kutoa semina elekezi kwa viongozi
wake katika ngazi za kata Wilaya na Mkoa, ili kuepusha mliangiliano wa utendaji kazi
ambao umekuwa ukitokea mara kwa mara na kupelekea migogoro ya mara kwa mara.
Akizungumza
na Jumuiya na wanawake jana mkoani hapa,
Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo nchini Gaudentia Kabaka, alisema baada ya kuona kuna
mgongano wa kuingiliana majukumu kati ya Wenyeviti pamoja na makatibu kitu
ambacho kinapelekea utendaji kazi kukwama.
“Tunawatoa
semina elekezi kwa wenyeviti,makatibu na wajumbe wa mabaraza kwanzia ngazi ya Kata,Wilaya
na Mkoa mada zitakazo wasilishwa ni Rushwa,malezi,uongozi bora pamoja na
ujasiliamali”,alisema.
Gaudentia
alisema wataalamu wa kutoa mafunzo hayo tayali wameandaliwa kwa ajili ya kutoa
mafunzo hayo.
“Haya
mafunzo ni ya nchi nzima lakini tunaenda Kanda kwa kanda ndiyo maana mwezi huu
tutanzia Nyanda za Juu Kusini na badae kuhamia sehemu nyingine”,.
Mwenyekiti
wa Ccm Mkoa wa Mbeya Jacob Mwakasole, alisema “Wananchi pamoja na wanachama wa
Ccm wanatamani kuona Ujio wa Rais wa Jamhuri ya Tanzania John Magufuli kuja
kuwasikiliza kero wanazokumbana nazo kwani tangu amechaguliwa hajafika kuongea
na wananchi wake, tunaomba mama Kabaka mfikishie kilio cha wananchi wetu”.
Mwakasole
alisema wananchi wa Mkoa wa Mbeya wamejawa na hamasa ya kumuona Rais baada
kuridhika na utendaji kazi mzuri tangu aingie madakani.
Katibu wa
Ccm Mkoa wa Mbeya Wilison Nkhambako alisema, Chama hicho kimeanza kujipanga kwa
ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu kwa kutembelea miradi
mbalimbali katika kila Wilaya na kugundua baadhi ya kasoro ambazo wataziwasilisha
kwa Mkuu wa Mkoa ili zipatiwe ufumbuzi mapema.
Mwisho.
Post a Comment