Header Ads

MADIWANI MBEYA DC WAPITISHA SH. 59 BILIONI BAJETI YA 2018/19


Mbeya. Baraza la madiwani Halmashauri ya Mbeya mkoani hapa limepitisha bajeti ya Sh 59 bilioni kwa mwaka wa fedha 2018/19 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali katika halmashauri hiyo.
Akiwasilisha  bajeti hiyo jana Ofisa Mipango wa Halmashauri hiyo Filbert Mbwilo ,alisema vipaumbele vikubwa katika bajeti hiyo ni ujenzi wa Shule ya wasichana Garijembe pamoja na Machinjio ya kisasa eneo la Utengule Usongwe.
 Mbwilo alisema katika mwaka wa fedha ujao Halmashauri imejipanga kusimamia, kukusanya mapato kutoka vyanzo vya ndani pamoja na vyanzo vingine vitakavyofanya wafikie malengo ya bajeti hiyo.
Alisema katika bajeti hiyo ,vipaumbele vikubwa ni kutengeneza machinjio ya kisasa itakayogharimu zaidi ya Sh 200 milioni huku vipaumbele vingine vikiwa ni kuboresha miundombinu ya elimu, afya ,elimu maji  na vinginevyo. 
“Lakini pia mwaka huu tumejipanga  kudhibiti upotevu wa mapato katika kata zetu tunatarajia kununua pikipiki kwa watendaji wa kata na vijiji ili iwe rahisi kufikia maeneo ya vijijini kukusanya mapato na tozo mbalimbali zinazotoka kwa wakulima na wafanyabishara, ‘’alisema.
Akichangia  bajeti hiyo, Diwani wa kata ya Bonde la Songwe ,Ayasi Ramadhani, alisema katika mwaka wa fedha uliyopita kulikuwa changamoto ya ukusanyaji wa mapato kutokana na mazao ya mahindi, viazi na pareto kukosa soko na kwamba halmashauri hiyo inapata fedha zake kutoka katika mageti yanayovusha mazao hayo.
Diwani wa viti maalum Frola Lucas,alisema ‘Katika mwaka wa fedha ujao naomba halmashuri yetu ibadilike katika kukamirisha miradi ya awali ndipo tuanze upya kutokana na kwamba tunamiradi mingi ambayo mpaka sasa kwa asilimia kubwa haijakamilika kutokana na usimamizi mbovu”.
Alitoa mfano miradi zaidi ya minne ya maji ambayo tangu mwaka 2013 hadi  sasa haiujakamilika na kwamba kutokamilika kwa miradi hyo kunachangia kucheleweshwa utekelezaji wa miradi mipya kwa wananchi.
Kwa Upande wake mwenyekiti wa Halmnashauri hiyo,Mwalingo Kisemba aliungana na madiwani hao kupitisha bajeti hiyo na kumuomba Mkurugenzi kwa kushirikiana na kamati ya fedha kuangaliua namna ya kukopa fedha kutoka taasisi yoyote ili waweze kununua gari za kubeba taka katika halmashauri hiyo.
‘’Ni aibu kuona halmashuri nzima hatuna gari hata moja kwa ajili ya kubeba taka na ndiyo maana magonjwa ya mlipuko yanatukumba mara kwa mara kutokana na hili hebu mwaka huu mpya wa bajeti tuje kivingine,’’alisema Kisemba.
Mwisho.

No comments