Header Ads

Wazee 9,679 Mkoa wa Mbeya wameandikishwa na kupewa kadi kwa ajili ya matibabu bure.


Mbeya. Wazee 9,679 Jijini hapa wameandikishwa na kupewa kadi kwa ajili ya   matibabu bure katika vituo vya afya na zahanati zilizopo ndani ya jiji kulingana  na sera ya afya inavyo sema.

Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili Ofisa ustawi wa jamii jiji la Mbeya Eva John alisema zoezi la uandikishaji wa wazee bado unaendelea katika mitaa mbalimbali ili kuhakikisha kila mzee anapata kadi hiyo huduma za matibabu bure.

Eva alisema changamoto kubwa ni baadhi ya wazee  hao bado hawajahamasika kujitokeza maeneo tuliotenga kuja kuandikisha ili kupata vitambulisho ambavyo vinatakiwa vionyeshwe sehemu ambapo watapatiwa huduma za matibabu.

“Changamoto kubwa tulio nayo hapa ni kwamba wazee walipo jijini hapa bado hawajahamasika kuja kwenye vituo vilivyo tengwa na watendaji wa kata kujiandikisha hivyo inapelekea baadhi yao kuto kupewa kadi hizo kwa ajili ya matibabu bure”,alisema.

Eva aliongeza kuwa “Hata kama mzee hana kadi akienda kituo chochote atapatiwa matibabu bure kulingana na umri alionao ili mradi tu awe anaishi ndani ya jiji”,alisema.

Mkazi wa majengo jijini hapa Ambangile Mwambusye,alisema kwa sasa dirisha la wazee kwa ajili ya matibabu bure limekuwa likifanya huduma nzuri tofauti na awali.

“Tunaipongeza  serikali kwa kusimamia hudumu ya matibabu bure kwa wazee kwa kweli huduma zimeboreshwa kwa hali ya juu sasa hivi nimetoka kituo cha afya Kiwanja mpaka wamenihudumia vizuri na nimepewa kipaumbele cha kuhudumiwa”,alisema.

Naye Brown Ambindwile mkazi wa kata ya Ghana alisema licha kupewa kadi kwa ajili ya matibabu bure lakini tatizo la uhaba dawa katika vituo vya afya na zahanati tunavyo hudumiwa ni changamoto kubwa.

“Tunaomba serikali kuongeza dawa katika vituo vya afya na zahanati kwani kuna mda tunakosa kabisa hapa tunaambiwa tukanunue wakati huo sisi pesa hatuna hivyo inatuwia vigumu sana kutafuta pesa ya kununulia madawa ambayo tunandikiwa na watalam wetu”,alisema.

No comments